MAUAJI YAENDELEA NYAMONGO

Wavamizi { intruders} wakijaribu kupambana na maaskari polisi na walinzi wa kampuni YA ABG NORTH MARA nyamongo tarime


Watu wawili wameuwawa kwa kupigwa risasi na jeshi la polisi kanda maaluum ya Tarime na Rorya  kwa tuhuma ya  kuvamia mgodi wa kuchimba Madini ya  dhahabu wa barrick North Mara uliopo nyamongo wilayani Tarime Mara

Akiongea na wandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa jeshi la polisi kanda maalum ya tarime na rorya  ACP Justus Kamgisha ameeleza kwamba mnamo tarehe 30/08/2012 kuanzia mida ya saa 12 jioni hadi saa  moja jioni watu wanao kadiliwa kuwa kati ya 800 au 1000  kwa jina maarufu intruders walivamia mgodi wa ABG North Mara uliopo katika vijiji vya kewanja na nyangoto  maeneo la rampad na shimo la Gokona wakiwa na slaa za jadi kama vile mapanga nyundo mawe na rungu  wakiwa na nia ya kupora dhahabu na kuwashambulia askari polisi walio kuwa doria  katika maeneo hayo

Kamanda kamgisha  ameeleza kuwa katika jitihada ya kuwazuia wavamizi hao askari na E6059 D /COPLO JULIUS alikatwa panga usoni na  na mgongoni na kuanguka ndipo askari wengine katika jitihada za kumuokoa askari huyo wavamizi {INTRUDERS} wawili PAUL SARYA miaka 26 wa  wa kiji cha nyangoto na RODGERS MWITA miaka 18 wa kijiji cha kimusi  walipigwa Risasi na kufariki

Kwa upande wake mganga mfawidhi  wa hospitali ya wilaya ya tarime DR Nega Marco amekiri kupokea maiti wawili na majeruhi mmoja ambae ni Mseti Chacha  miaka 20 mkazi wa nyamwaga

Pia jeshi la polisi kanda maalum ya tarime rorya imetoa rai kwa wananchi  kwa kuwataka watii sheria bila shuruti kwa kuacha kuvamia mgodi huo kwa nia ya kupora mawe yenye dhahabu

 tabia na vitendo vya kuvamia mgodi wa abg north mara vimekuwa vikijirudia mara kwa mara na kusababisha baadhi ya wananchi wengi kupoteza maisha wakiwemo raia, walinzi wa mgodi na baadhi ya askari polisi kujeruhiwa vibaya na wavamizi  {INTRUDERS} ni vyema  sasa serikali ikaangalia upya  nanma ya kusaidia  na kutatua tatizo hili linalogusa zaidi wananchi wa wilaya ya tarime na watanzania wote kwa ujumla..

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KIJIJI CHA KERENDE CHAKABIDHIWA BARABARA YA TSH MILIONI 26-TARIME

VIONGOZI WANAO HAMASISHA KILIMO CHA BANGI KUCHUKULIWA HATUA