NA JUMANNE  NTONO – MUGUMU SERENGETI MARA

            0786 992 552 / 0763 992 552 / 0715 992 552


Wakati zoezi la kukusanya maoni ya katiba likiendelea mkoani mara wananchi wa wilaya ya Serengeti mkoani humo wameaswa kujitokeza kwa wingi  ili kutoa maoni yao

Wito huo umetolewa na mwenyekiti wa vijana wa chama cha demokrasia na maendeleo chadema   mkoa wa mara bw chacha heche  wakati wa kufungua ofisi ya tawi jipya la chadema katika stendi yaw mugumu

Bw chacha   amewataka wananchi hususani vijana waakikishe  wanajitokeza kwa wingi katika zoezi la kukusanya maoni kwa wananchi ili watoe mawazo yawo ya msingi hususani tatizo la ardhi ambayo imekuwa na migogoro  mikubwa hapa nchini  na kusababisha baadhi ya wananchi kuonekana kana kwamba ni wakimbizi katika nchi yao

Pia bw chacha  ameeleza kwamba jukumu la  kuleta maendeleo katika nchi hii nila kila mwananchi  kwa hiyo  wananchi watoe maoni yao yanayo lenga maendeleo ya watanzania ikiwemo kulejesha viwanda  na mashirika ya umma yaliyo kufa kwa  sababu ya uzembe wa watu wachache walioko madarakani

 Kwa upande wake diwani wa kata ya stendi kuu ya mugumu bw rioba marwa amewaeleza wananchi  kwamba madiwani walio wachagua siyo wawakilishi wa wananchi bali niwafanya biashara walio chaguliwa kufanaya biashara na  halmashauli.  miradi mingi  inayo tekerezwa katika halmashauli hiyo  ina ubora wa chini na  sii  ya kiwango kilicho kusudiwa. kwa sababu  tenda nyingi za miradi hiyo kuchukuliwa na madiwani wa halmashauli hiyo. hali ambayo husababisha  usimamiaji wa miradi hiyo kuwa mgumu na ukizingatia wasimamizi na wakaguzi wa miradi hiyo ni haohao madiwani   wenye tenda.

Sambamba na ufunguzi wa tawi hilo chadema wanatarajia kufugua  matawi mengi zaidi  katika kila kata na kila kijiji wilayani Serengeti.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KIJIJI CHA KERENDE CHAKABIDHIWA BARABARA YA TSH MILIONI 26-TARIME

MAUAJI YAENDELEA NYAMONGO

VIONGOZI WANAO HAMASISHA KILIMO CHA BANGI KUCHUKULIWA HATUA