NA JUMANNE NTONO - TARIME MARA
                        05/12/2012
      0786 992 552 / 0763 992 552 / 0715 992 551

Wazee wa mila tarime wameyataka mashirika mbalimbali ya yanayo  toa elimu kuhusu  kutokomeza  ukeketaji  kwa mtoto wa kike  tarime  yaache tabia ya kuwatumia kama vitega uchumi vyao na badara yake walete mabadiriko kwa jamii

Hayo yalielezwa na viongozi wa wazee wa mila kutoka koo 13 za kabila la wakurya walio kuwa  kwenye mafunzo  na majadiano ya kutafuta ufumbuzi wa kutokemeza suala la ukeketaji  kwa watoto wa kike wilayani humo mafunzo yaliyoandaliwa na shirika la utu wa mtoto CDF

 Wazee hao wamekuwa na ofu  na kusababisha wadai  kwamba pengine baadhi ya mashirika yanayo kuja kuielimisha jamii kuhusu jambo hilo na kuwaita  watu wachache katika kumbi za mjini wakiwemo wazee  wa mila wachache  yanawatumia wazee hao kama mitaji yao ya  kuombe pesa  kutoka kwa wafadhiri mbalimbali  wanao wasaidia lakini siyo kuja kumaliza tatizo la ukatiri kwa mtoto wa kike    


Kwa upande wake  mkuu wa wilaya ya tarime bw john henjewele ameeleza kwamba pamoja na kutoa mafunzo mbalimbali kuhusu madhara ya ukeketaji  kwa jamii. serikali kupitia halmashauli  ya wilaya ya tarime kwa sasa wana tarajia kuanza  ujenzi wa  shule ya sekondari   ya wasichana katika kijiji cha borega  kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita wilayani tarime

Pia mkurugenzi wa shirika la utu wa mtoto[ cdf]  bw konshuma  mtengeti. Amesema kwamba pamoja na changamoto zinazo wakabili .  kupitia shirika lao  wataendelea kuisapoti jamii katika kutoa elimu  kuhusu madhara ya ukeketaji kwa mtoto wa kike na amewaomba wananchi  viongozi wa chama na serikali  waendelee kuwapa ushirikiano katika masuala ya ukeketaji kwa mtoto wa kike.


Na katika kipindi hiki cha mwezi wa kumi na mbili zaidi ya koo kumi kati ya koo kumi na tatu za kabila la wakurya wilayani tarime  wanatarajia kukeketa watoto wa kike zaidi ya miatatu



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KIJIJI CHA KERENDE CHAKABIDHIWA BARABARA YA TSH MILIONI 26-TARIME

MAUAJI YAENDELEA NYAMONGO

VIONGOZI WANAO HAMASISHA KILIMO CHA BANGI KUCHUKULIWA HATUA