NA JUMANNE NTONO

0786 992 552/ 0763 992 992/ 0715 992 552

12/12/2012

Umoja wa makanisa ya kikristu   tanzania cct na watoto wa kike wametoa tamko la  kukataa ukeketaji wilayani  tarime

Tamko hilo limetolewa na mkuu wa dayosisi ya  Tarime kanisa la menonite tanzania mchungaji ANDREW RYAGA  kwa niaba ya cct wilaya ya Tarime na watoto wa kike  katika kongamano la kukataa  na kupinga vitendo vya  kikatiri na  vya unyanyasaji kwa watoto wa kike lililo fanyika katika kijiji cha Kemakorere wilayani  Tarime

Wakitoa tamko hilo mchungaji ANDREW  RYAGA  amesema kwamba mtu yoyote atakae bainika akijiusisha na vitendo vya ukeketaji kwa watoto wa kike  mwaka huu achukuliwe hatua kwa kukeuka agizo la serikali na madhehebu  yote ya dini ya kikristo Tanzania.watoto wa kike nao wakawataka viongozi wa serikali watoe agizo kwa wale wanao keketa  watoto wa kike kama walivyo toa agizo kwa walio jiusisha na ukatwaji wa viuongo vya walemavu wa ngozi Maalbino

Nao baadhi ya wazazi walio hudhuri tamasha hilo lililo shirikisha zaidi watoto  wa kuanzia miaka tisa hadi kumi na tano  ambao wengi wao ndio wanarengwa kukeketwa kwa kipindi hiki cha mwezi wa 12 mwaka huu wao wameitupia serikali lawama kwa kushindwa kuwachulia hatua za kisheria wale wote wanao jihusisha na vitendo vya ukeketaji huku wakiwaona kwa macho  yao wakifanya sherehe za ukeketaji kwa watoto wa kike

Kwa upande wake mgeni rasmi wa tamasha hilo katibu tarafa wa tarafa ya inchage wilayani tarime BW JONATHAN MACHANGO amewaeleza wananchi kuwa badara ya kuchangia sherehe kwa ajiri ya ukeketaji kwa mtoto wa kike sasa wachangie elimu kwa watoto hao ili wapate elimu itakayo wasaidia katika maisha yao ya badae


Mapema mratibu wa tamasha hilo mchungaji JOSEPH MAHUGIJA alieleza kwamba lengo la tamasha hilo ni kutoa elimu kwa  jamii ili  iachane na vitendo vya ukatiri wa kijinsia kwa wanawake na watoto.  

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KIJIJI CHA KERENDE CHAKABIDHIWA BARABARA YA TSH MILIONI 26-TARIME

MAUAJI YAENDELEA NYAMONGO

VIONGOZI WANAO HAMASISHA KILIMO CHA BANGI KUCHUKULIWA HATUA