michezo

Hatimae timu ya polisi tarime mkoani mara imeibuka bingwa wa  ligi ya amani  mahusiano cup  kwa mpira wa miguu na wa pete     

Timu hiyo ya polisi iliyo ingia fainali na timu ya kijiji cha matongo  imeibuka  bingwa wa mpira wa miguu  kwa wanaume kwa kuifunga  magori matatu kwa bila  pia  imekuwa bingwa wa mpira wa pete kwa wanawake kwa kuifunga timu ya sodesco kwa magori 42 kwa 5

na baada ya fainali hizo kumalizika  katika viwanja vya sekondari ya nyamongo  makocha wa timu za polisi walisema kwamba siri ya ushindi wao ni maandalizi mazuri ya timu zao na ushirikiano mzuri kutoka kwa uongozi wa timu walimu na wachezaji

 huku kocha wa timu ya matongo BW JOSEPH MTOTO  akieleza kwamba timu yake imeshindwa kutwa kombe hilo kwa sababu ya wachezaji wake kuogopa jina la polisi


kwa upande wa wadhamini wa mashindano hayo shirika la search for common ground lililopo tarime na kampuni ya kuchimba madini ya dhahabu  ya African barrick gold{ north mara}wamewapongeza wananchi kwa ushirikiano walio utoa na namna walivyo hamasika  na kuonyesha ushirikiano katika suala zima la kujenga mahusiano kwa njia ya  michezo   

na wakaeleza kwamba  lengo la mashindano hayo ni kuwaweka pamoja  wadau mbalimbali kwa njia ya michezo ambao kwa njia nyingine wana muingiliano wa moja kwa moja na shughuli za uchimbaji wa dhahabu katika eneo hilo la nyamongo baina ya polisi jamii mwekezaji na serikali ili kujadili na kukumbushana wajibu wa kila mmoja wao kutambua tofauti zao na kuishi kwa makubaliano

katika mashindano hayo mshindi wa kwanza  mpira wa miguu aliibuka na kikombe mipira 4 na shilingi   laki nane huku  mshindi wa kwanza mpira wa pete akiibuka na kikombe  mipira mine na shilingi  laki tatu.

ligi hiyo ilishirikisha timu 40 za michezo mbalimbali ikiwemo  bao’ draft’ kufukuza kuku’ kuvuta kamba’ na kukimbia na maji kichwani

NAHODHA WA TIMU YA POLISI TARIME MPIRA WA MIGUU AKIPOKEA MOJA YA ZAWADI WALOZO PEWA

NAHODHA WA TIMU YA POLISI TARIME MPIRA WA PETE BI NYAMINGA AKIPOKEA KIKOMBE CHA UBINGWA WA AMANI MAHUSIANO -NYAMONGO

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KIJIJI CHA KERENDE CHAKABIDHIWA BARABARA YA TSH MILIONI 26-TARIME

MAUAJI YAENDELEA NYAMONGO

VIONGOZI WANAO HAMASISHA KILIMO CHA BANGI KUCHUKULIWA HATUA