WAZIRI WA KAZI NA AJIRA MH GAUDENSIA KABAKA AKIWAKABIDHI ZAWADI WAHITIMI 13 WA MAFUNZO YA TOHARA MBADARA WA KITUO CHA MASANGA WILAYANI TARME MARA
WAHITIMU 13 WA MAFUNZO MBADARA YA TOHARA AU UKEKETAJI WAKIIKMBA NYIMBO ZA FURAHA


Watakao vamia kituo cha kutoa elimu ya tohara mbadara kwa watoto wa kike  cha masanga   wilayani tarime mkoani mara kwa nia yakuvuruga Marengo ya kituo hicho  watashughulikiwa na serikali

Agizo hilo limetolewa  na waziri wa ajira na kazi BI  GAUDENSIA KABAKA
Kwenye sherehe ya kuhitimu mafunzo ya elimu mbadara  ya ukeketaji  kwa watoto wa kike iliyo fanyika katika kituo cha masanga wilyani tarime

BI GAUDENSIA amewaagiza viongozi wote  kuanzia ngazi ya kitongoji  hadi wilaya kuakikisha  walimu na watoto wote wa kike wanao pata elimu mbadara ya ukeketaji  katika  kituo cha masanga wanaishi kwa amani bila vitisho vyovyote kutoka kwa wananchi wa eneo hilo

 Pia mh gaudensia  ameiomba  kampuni ya  kuchimba madini ya dhahabu AFRICAN BARRICK GOLD NORTH MARA  iliyopo nyamongo wilayani tarime pamoja na majukumu  makubwa waliyo nayo  ya utekelezaji  wa  miradi mbalimbali  ya huduma za jamii. kama upo uwezekano basi ni vyema wakajengewa chuo cha ufundi katika mkoa wa  mara  ili kunusuru vijana wengi wa mkoa huo wanao hitaji kujiendeleza  katika fani mbalimbali za ufundi
  
Mapema akisoma risala ya chuo kwa mgeni rasmi BI EUNICE ANTHONY  amesema kwamba wao  hawana kituo cha kuhifadhi watoto wanao kimbia kukeketwa  bali wana kituo cha  kufundisha elimu mbadara ya ukeketaji inayo mfanya mtoto wa kike aweze kujitambua kimwiri na kiakili.


 Watoto  wa kike nao kupitia  risala yao wameitaka serikali iwachukulie hatua kali wazazi wanao watendea watoto wa kike vitendo vya  ukatili  

Toka mwaka 2008 hadi 2012 jumla ya watoto wa kike 642 wamehitimu mafunzo ya tohara mbadara katika kituo hicho  na kukabidhiwa kwa wazazi wao, huku wazazi hao wakitakiwa kuto wafanyia vitendo vyovyote vya kikatiri majumbani mwao.


HAWA NI BAADHI TU YA WATOTO WA KIKE WANAO ENDELEA KUPATA ELIMU YA TOHARA  MBADARA KATIKA KITUO  CHA MASANGA



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KIJIJI CHA KERENDE CHAKABIDHIWA BARABARA YA TSH MILIONI 26-TARIME

MAUAJI YAENDELEA NYAMONGO

VIONGOZI WANAO HAMASISHA KILIMO CHA BANGI KUCHUKULIWA HATUA