Hizi ni baadhi ya nyumba zilizo kabidhiwa kwa uongoizi wa
shule ya  sekondali ya ingwe- Tarime
kushoto kaimu meneja wa NORHI MARA Bw MARCK LUYT
 na mkurugenzi mtendaji wa Halmashauli ya wilaya ya Tarime
 Bw Athuman Akalama wakikata utepe na  kukabidhi nyumba 12
 kwa shule ya sekondali Ingwe- Tarime


Kampuni ya kuchimba madini ya dhahabu ya ABG NORTH MARA  iliyopo nyamongo wilayani tarime mkoani mara imekamilisha ujenzi wa nyumba kumi za kuishi zenye thamani ya shilingi milioni 685 za kitanzani  na kukabidhi kwa uongozi wa shule ya sekondali ingwe iliyopo nyamongo wilayani tarime

Akikabidhi nyumba hizo kwa mkurugenzi mtendaji wa Halmashauli ya wilaya ya Tarime Bw Athumani Akallama kaimu meneja wa kampuni hiyo BW   MARC LUYT  ameelza kwamba lengo la kampuni ni kuhakikisha inashirikiana na wananchi katika kuboresha huduma ya jamii hususani upande wa  elimu


Akipokea msaada huo mkurugenzi mtendaji wa Halmashauli ya wilaya ya tarime BW Athumani Akallama  ameipongeza kampuni hiyo na kueleza kwamba kampuni hiyo imesaidia mambo mengi katika wilaya hiyo katika  sekta ya elimu barabara afya na maji Na akawataka wananchi wa wilaya hiyo waendelee kutoa ushirikiano kwa kampuni hiyo  na kutunza miradi yote inayo tekerezwa na kampuni hiyo.


Bw Tanzania Omtima ambae ni mwenyekiti wa kijiji cha kewanja na Bw Wilson Mangule diwani wa kata ya kemambo pamoja na kuishukuru kampuni hiyo kwa kuwajengea nyumba kumi za walimu. wameitaka kampuni hiyo iendelee kuisaidia shule hiyo  kwa kuwajengea uzio katika shule hiyo na kuwawekea umeme ili kunusuru wanafunzi wengi wanao kumbana na vishawishi vya  pesa nyingi inayo toka  katika mgodi huo wa NORTH MARA

Kampuni hiyo inaendelea na ujenzi vyumba  vinnne vya mahabara katika shule hiyo ikiwa na lengo la kuboresha shule hiyo kuwa ya kisasa zaidi ikiwezekana iwe shule ya mfano katika mkoa wa mara.


………………………………..mwisho…………………………………………………….



vingozo  wakiangalia nyumba zilizo kabidhiwa kwa uongozi wa shule ya sekondali ingwe - Tarime

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KIJIJI CHA KERENDE CHAKABIDHIWA BARABARA YA TSH MILIONI 26-TARIME

MAUAJI YAENDELEA NYAMONGO

VIONGOZI WANAO HAMASISHA KILIMO CHA BANGI KUCHUKULIWA HATUA