NEW LIFE CHRIST WAENEZA INJIRI MARA



Ili kupunguza mambukizi mapya ya virusi vya  ukimwi  wilayani  Rorya mkoani Mara wananchi wametakiwa kuepukana na mira potofu na kumrudia mungu


  Wito huo umetolewa na mwenyekiti wa umoja wa makanisa ya kikristo  mkoa wa dar es salaam mchungaji  HALSON MUMANYI kwenye hitimisho la mahubiri ya siku nane yaliyo endeshwa na shiriks la NEW LIFE CHRIST katika wilaya ya  Tarime na Rorya mkoani Mara
  
Mwenyekiti Halson ameeleza kwamba wilaya ya Rorya inamaambukizi makubwa ya virusi vya ukimwi kutoka na wananchi wengi wa wilaya hiyo kuto mrudia  mungu


 Pamoja na watu kumrudia mungu mwenyekiti huyo amewataka wananchi  wa wilaya ya Rorya na Tarime waache  tabia ya kurithi wake wa marehemu { wajane} kwa madai kwamba wanadumisha mira, kwa kuwa mira hiyo   imepitwa na wakati na haina tija tena kwa jamii

Nao baadhi ya wananchi na viongozi mbalimbali walio hudhuria mahubiri hayo wamesema kwamba mahubiri ya siku nane yatawaimarisha kiroho 


Kwa takwimu za mwaka 2012 wilaya ya rorya ni ya kwanza kimkoa kwa kuwa na maambukizi ya asilimia 6.2  


………………………mwisho…………………………………….

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KIJIJI CHA KERENDE CHAKABIDHIWA BARABARA YA TSH MILIONI 26-TARIME

MAUAJI YAENDELEA NYAMONGO

VIONGOZI WANAO HAMASISHA KILIMO CHA BANGI KUCHUKULIWA HATUA