DC NA MBUNGE WAONDOA TOFAUTI ZAO WAJIKITA KATIKA MAENDELEO- RORYA

MKUU WA MKOA WA MARA JOHN GABRIEL TUPA AKIONGEA KWENYE KIKAO CHA USURUHISHI KATIKA UKUMBI WA SOHA HOTEL UTEGI RORYA 
[

TUPA AMALIZA MGOGORO WA DC NA MBUNGE- RORYA]

Hatimae mgogoro mkubwa wa kutoelewana   kwa viongozi wawili wa ngazi ya juu katika wilaya ya rorya mkoani mara  ulio kuwa umeibuka hivi karibuni na kusababisha  kukwama kwa shughuli za maaendeleo kwa wananchi huku wananchi wakibaki na  kitendawili cha sintafahamu hatimae umemalizika

DC wa Rorya Elias Goroi akiongea katika
mkutano wa kikao cha usuruhishi
Huku viongozi hao kwa pamoja wakihaidi kushirikiana kwa pamoja katika kuwaletea wananchi wa rorya maendeleo
  
Viongozi hao ambao ni mkuu wa wilaya ya rorya bw Elias Goroi na mbunge wa jimbo hilo bw Lameck Airo kwa pamoja  na mbele ya kikao kilicho itishwa na mkuu wa mkoa mara bw John Gabriel Tupa  katika mji mdogo wa utegi na kushirikisha wazee maarufu wa wilaya rorya na viongozi wa madhehebu ya dini viongozi hao wameondoa tofauti zao na  kusem kwamba watashirikiana kwa pamoja katka kuijenga Rorya 

Kitendo cha viongozi hao kukubaliana na kuondoa tofauti zao kimepongezwa na wazee na vingozi wa dini na kuwataka waliyo yasema yawe yametoka moyoni mwao kama walivyo tamka wenyewe alisema mzee Kembo Migire na askofu wa kanisa la mennonite John Nyagwegwe





kushoto Lameck Airo mbunge rorya akiongea  kwenye kikao cha
usururhishi wa mgogogro wa dc na mbunge 

Akifunga kikao hicho mkuu wa mkoa wa mara bw John Gabriel Tupa ametoa wito kwa viongozi wote wa mkoa mara wawe na tabia ya kuwa na vikao vya mara kwa mara vitakavyo wasaidia kubaini baadhi ya changamoto zinazo wakabili na kuzitatua kwa wakati bila marumbano

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KIJIJI CHA KERENDE CHAKABIDHIWA BARABARA YA TSH MILIONI 26-TARIME

MAUAJI YAENDELEA NYAMONGO

VIONGOZI WANAO HAMASISHA KILIMO CHA BANGI KUCHUKULIWA HATUA