[KANISA LA KKKT LALAANI MAUAJI TARIME}

Kanisa la kiinjiri la kirutheri Tanzania dayosisi ya mkoani mara limelaani mtu au kundi lililo fanya mauaji ya watu nane katika mji wa tarime na kusema mungu hapendezwi na matukio ya haina hiyo na kwa kupitia maombi mtu au watu walio fanya matukio hayo  watabainika  

Hayo yameelezwa na askofu wa kanisa la kkkt dayosisi ya mkoani mara askofu Michael Adam kwenye ibada ya mazishi ya daudi  mwasi  alie zikwa katika kijiji cha nyamwaga wilayani tarime , ambae ni mmoja kati ya watu 8 walio uawa  usiku wa tarehe 27 january 2014 kwa kupigwa risasi na watu au mtu asie julikana

Askofu Michael  amesema kwamba  kwa ushirikiano wa maombi sala vyombo vya dora na raia wema ana amini waharifu au mharifu  huyo atakamatwa na sheria kuchukua mkondo wake


Pia baadhi ya wananchi walio shiriki katika mazishi hayo akiwemo mbunge msitaafu wa jimbo la tarime Charles Mwera , diwani wa kata ya Nyamwaga Wambura Nyagare  na John Rotente  nao wamelaani mauaji hayo na kuwataka wananchi watoe ushirikianao kwa jeshi la polisi katika kufanikisha zoezi la kuwabaini wahusika wa matukio hayo




………………………………….MWISHO………………………………………

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KIJIJI CHA KERENDE CHAKABIDHIWA BARABARA YA TSH MILIONI 26-TARIME

MAUAJI YAENDELEA NYAMONGO

VIONGOZI WANAO HAMASISHA KILIMO CHA BANGI KUCHUKULIWA HATUA