NYUMBA YATEKETEA KWA MOTO TARIME

NYUMBA pamoja na vyombo vya ndani vya Naftari Philipo Akyoo mkazi wa mtaa wa bomani katika Halmashauri ya mji wa Tarime mkoani mara imeteketea kwa moto unaodhaniwa kuwa chanzo chake kimetokana na shoti ya umeme wa Tanesco 


akiongea katika eneo la tukio la nyumba kuungua moto,mmmiliki wa nyumba hiyo Naftari Philipo Akyoo anasema kabla ya siku nne kutokea kwa tukio hili,alitoa taarifa ya tatizo la umeme wa nyumba hiyo katika ofisi ya Tanesco wilaya yaTarime na wakafika kuona tatizo, lakini kabla ya kuja kutatua tatizo hili ,nyumba ikawa Tayari  imeungua


nao baadhi ya mashuhuda wa tukio hili ambao ni mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa bomani Marema Solo, na diwani wa kata ya bomani Godfrey Masubo,wao wakaelekeza  lawama zao kwa uongozi wa Halmashauri ya mji wa Tzarime kwa kushindwa kununua  gari la zima moto

wilaya ya Tarime inao askari wa jeshi la zima moto lakini jeshi hili halina gari la kuzima moto
mwisho 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KIJIJI CHA KERENDE CHAKABIDHIWA BARABARA YA TSH MILIONI 26-TARIME

MAUAJI YAENDELEA NYAMONGO

VIONGOZI WANAO HAMASISHA KILIMO CHA BANGI KUCHUKULIWA HATUA